Jamhuri ya Afrika ya Kati (Kifaransa: République Centrafricaine/ʀepyblik sɑ̃tʀafʀikɛn/ ama Centrafrique/sɑ̃tʀafʀik/) ni nchi Bara bila pwani Kati ya afrika. Imepakana na Chadi kaskazini, Sudan mashariki, Jamhuri ya Kongo na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo upande wa kusini na Kamerun upande wa Magharibi. Nchi hii, hasa ina shikilia eneo tapakaa Sudani-Guinea savanna, na pia jangwa la Sahara eneo ya kaskazini na eneo ya msitu wa ikwete kusini. Theluthi mbili za eneo ya nchi hii zimetapakaa kwa Mabia ya mto Ubangi unao tiririka kusini kwa Mto Kongo, na theluthi ya eneo katapakaa kwa mabia ya mto Shari, unao tiririka kusini kwa Ziwa Chadi. Kwa sababu ya Utapakazi wa eneo kwa mabia ya mto Ubangi na mto Shari, Wafaransa wakati wa ukoloni waliita nchi hii Ubangi-Shari, ama Oubangui-Chari kwa kifaransa. Ilipokua koloni ya Ufaransa, Ubangi-Shari ziliwekewa mamlaka ya madaraka kama eneo ya Jamii ya Wafaransa mwaka wa 1958 lakini baadaye kupata Uhuru Agosti 1960. Kwa miaka mlongo tatu kutioka Uhuru, ‘Jamhuri ya Afrika ya Kati’ ilitawalwa na serikali za nguvu zilizo nyakua mamlaka bila demokrasia, lakini mwaka wa 1993, Kura za Demokrasia za kwanza zilifanywa na kumchagua Ange-Félix Patassé kuwa Rais. Lakini Rais Patassé alipenduliwa na Jenerali François Bozizé mwaka wa 2003. Jenerali Bozizé alishinda kura za kidemokrasia manamo Mai 2005 na kuiongoza nchi mbaka wa sasa.